IQNA

Tamasha la kimataifa la filamu za matukio ya kweli ya Gaza laanza

20:18 - December 08, 2010
Habari ID: 2044823
Tamasha la pili la kimataifa la filamu za matukio ya kweli (documentary) katika Ukanda wa Gaza lilianza jana kwa ujumbe wa kushikamana na wananchi wa Palestina. Tamasha hilo linazikutanisha pamoja nchi 14 za Kiarabu na kigeni.
Kituo cha upashaji habari cha al Kauthar kimeripoti kuwa Waziri wa Utamaduni wa serikari halali ya Palestina Usama al Isawi amesema kuwa zaidi ya filamu 70 zimewasilishwa katika tamasha hilo.
Amesema kuwa ujumbe wa nchi zinazoshiriki katika tamasha hilo ni mshikamano na wananchi wa Palestina na kwamba kuna matumaini kwamba mfungamano huo utaendelezwa katika siku zijazo.
Katika upande mwingine Mustafa Hijazi ambaye ni mwanaharakati wa vyombo vya habari wa Palestina amesema kuwa filamu za tamasha hilo zinasimulia na kufichua jinai zinazofanywa na Wazayuni wa Israel dhidi ya raia wasiokuwa na hatia wa Gaza.
Sherehe za ufunguzi wa tamasha hilo zimehudhuriwa na wasanii na wanahabari wa Palestina na nchi za Kiarabu. 709354
captcha