IQNA

Magaidi wa ISIS wanaelekea wapi?

0:20 - January 24, 2016
Habari ID: 3470081
Mamia ya magaidi wa ISIS au Daesh wanatoroka Iraq na Syria wakielekea Libya ili kujiunga na wapiganaji wa kundi hilo la wakufurishaji Afrika Kaskazini.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, ukosefu wa serikali ya kitaifa Libya sambamba na kuwepo utajiri wa mafuta ni nukta ambazo zimepelekea vinara wa kundi la kigaidi la ISIS kuelekea katika nchi hiyo ya Afrika Kaskazini.
Baada ya kuanguka utawala wa dikteta Gaddafi mwaka 2011, nchi hiyo iligeuka na kuwa medani ya mapigano baina ya makundi mbali mbali ya wanamgambo na makundi ya magaidi wakufurishaji nchini humo. Hivi sasa magaidi wa ISIS wanadhibiti miji kadhaa  ya pwani ya Libya kama vile Sirte, Bin Jawad, na Derna.
Hivi karibuni iliripotiwa kuwa  magaidi 500 wa ISIS walionekana wakielekea Libya. Miezi miwili iliyopita Umoja wa Mataifa ulichapisha ripoti iliyobaini kuwa kuna magaidi 3000 wanaoendesha oparesheni zao za kihalifu nchini Libya. Duru nchini Libya zinataja idadi hiyo kuwa takribani 10,000.
Mwaka 2015,  idadi kubwa ya magaidi wa ISIS  nchini Libya walijiunga na kundi la wanamgmabo wanaojiita Ansar Sharia. Wanamgambo hao wametangaza utiifu wao kwa ISIS. Katika wiki za hivi karibuni pia, makundi mengine mawili yaani, "Baraza la Kimapinduzi la Ajdabiya" na kundi jingine la wanamgmabo huko Misrata walitangaza kujiunga na ISIS.
Wakuu wa Libya wanasema magaidi wa ISIS wanalenga kuteka vituo vya uzalishaji mafuta nchini humo. Siku chache zilizopita, vituo viwili vya kuuza mafuta ghafi ya petroli ya Libya katika masoko ya kimataifa vya Es Sider na Ra's Lanuf vilishambuliwa na magaidi wa ISIS.
Kundu la kigaidi la ISIS linalenga kudhibiti vituo vya mafuta Libya ili kuweza kupata pato kama ilivyo huko Iraq na Libya. Kukosekana serikali yenye nguvu Libya pamoja na mapigano ya ndani ni mambo ambayo yametoa mwanya kwa ISIS kujipenyeza Libya. Imearifiwa kuwa magaidi wa ISIS wamekimbilia Libya baada ya kupata pigo Syria na Iraq kufuatia mafanikio ya majeshi ya nchi hizo.
3469535
captcha