Ayatullah Khamenei amegusia pia mijadala iliyotawala kampeni za uchaguzi wa rais nchini Marekani kuhusu uharibifu, umaskini na matatizo mengi yaliyopo nchini humo na kusema: katika miaka ya hivi karibuni Marekani imetumia fedha za watu wa nchi hiyo katika vita visivyokuwa sharifu na matokeo yake ni mauaji ya makumi ya maelfu ya raia na kuharibiwa miundombinu katika nchi kama Afghanistan, Iraq, Libya, Syria na Yemen.
Vilevile ameashiria matokeo ya uchaguzi wa rais wa Marekani na kusema: Iran haina hukumu ya aina yoyote kuhusu uchaguzi huo kwa sababu Marekani bado ni ileile na chama chochote kilichoshika madaraka nchini humo katika kipindi cha miaka 37 iliyopita kati ya vyama viwili vya Republican na Democratic hakikuwa na kheri kwetu sisi na daima shari yao imekuwa ikilifikia taifa la Iran.
Ayatullah Khamenei amesema kinyume na baadhi ya watu duniani ambao
wamepatwa na majonzi kutokana na matokeo ya uchaguzi wa rais wa Marekani
au wale wanaofurahia matokeo hayo, sisi hatuko kwenye msiba wala
hatuyafurahii kwa sababu hakuna tofauti kwetu sisi na wala hatuna
wasiwasi, na kwa baraka zake Mwenyezi Mungu tuko tayari kukabiliana na
lolote linaloweza kutokea.