Mkuu wa Idara ya Utamaduni ya Iran katika mji mkuu wa Uganda, Kampala
Ali Bakhtiari katika mahojiano maalumu na IQNA, amesema, harakati za Qur'ani za
idara hiyo nchini Uganda zimejikita katika masuala ya kuelimisha na
kuandaa mashindano ya Qur'ani.
Ameongeza kuwa, aghalabu ya harakati za Qur'ani za idara hiyo katika
kipindi cha mwaka moja uliopta ni kuunga mkono mashindano ya Qur'ani
katika viwango mbali mbali vya kitaifa, vyuo vikuu, na shule.
Bakhtiari ameongeza kuwa, Idara ya Utamaduni ya Iran nchini Uganda mbali
na kushiriki katika harakati a Qur'ani katika vituo vya kidini na
Qur'ani kila mwaka idara hiyo huandaa mashindano ya Qur'ani katika
kiwango cha kitaifa kwa ushirikiano na Televisheni ya Kitaifa ya Uganda,
UBC, na mwaka huu pia mashindano hayo yanafanyika.
Ameongeza kuwa, mashindano hayo yatarushwa hewani moja kwa moja katika
katika kanali mbili za UBC. Bw. Bakhtiari amesema mashindano hayo ya
Qur'ani katika televisheni yatahudhuriwa pia na qarii wa kimataifa
pamoja na kundi la waimbaji qasida kutoka Iran.
Aidha amesema Idara ya Utamaduni ya Iran inashirikiana na televisehni ya
Kiislamu ya Salam TV katika kurusha hewani vipindi vya tafsiri na
ufahamu wa Qur'ani Tukufu.
Aidha amesema idara hiyo ya utamaduni inashirikiana na taasisi mbali
mbali za Kiislamu nchini Uganda huku masuala harakati za Qur'ani, umoja
baina ya Waislamu, amani duniani, vijana na wanawake yakipewa
kipaumbele.
3501564