Trump majuzi alisema kuwa kundi la ISIS/Daesh lilibuniwa na Rais Barack Obama wa Marekani kwa ushirikiano wa karibu na Hillary Clinton, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ambaye kwa sasa anagombea kiti cha urais kwa tiketi ya Democrats.
Tarehe 12 Julai mwaka 2006 jeshi la Israel lilishambulia ardhi ya
Lebanon kwa muda wa siku 33 na halikufanikiwa kufikia hata lengo moja
katika mashambulizi hayo kutokana na mapambano ya kishujaa ya
wanamuqawama wa Hizbullah. Wananchi 1,200 wa Lebanon aghalabu yao wakiwa
raia wa kawaida waliuawa huku Wazayuni 160 akthari yao wakiwa ni askari
vamizi wa utawala ghasibu wa Israel wakiangamizwa katika vita hivyo.